Search This Blog

Sunday, July 24, 2022

STYLE 8 BAO 1

    

MTUNZI : GEOFREY MALWA




Ndugu zangu, wapendwa wangu, sina ya kuwaogopesha juu ya wanawake. Ninaweza nikawa ni mmoja tu mpumbavu, naam mpumbavu ndio.

Naitwa Rozi, nina mwaka wa nne sasa katika ndoa yangu. Sijui nikikwambia kuwa nilimpenda mume wangu kupita maelezo utaniamini? Natumaini huwezi kuniamini kwasababu akilini mwa wengi huamini kuwa usipochepuka ndio unampenda mwenzio. Kweli niliwahi kuchepuka lakini sikuwahi kujutia, sikujutia na siwezi kusahau japo sitoweza kurudia tena kuchepuka.

Kujuta kwenye kuchepuka kunatokana na huko ulikochepukia, ukipelekewa moto wa maana huwezi kujutia. Pia unaweza kujutia kama mume wako ataendelea kukuonyesha upendo mkubwa, lakini kwangu nilionyeshwa upendo mkubwa baada ya kuchepuka ila sikuwahi kujuta.

Acha niwasimulie jinsi ilivyokuwa. Mimi kwakweli sio mtu wa kuchangamana sana na watu, tabia yangu hiyo ilimpendeza mume wangu lakini baadaye aliona kuna haja ya mimi kuwa na rafiki wa kuzungumza naye.

Kwa mume wangu sikukosa chochote, narudia tena sikukosa chochote, nilipewa kila moyo wangu ulichohitaji, kwenye hii dunia mume wangu namuweka nambari moja kati ya wanaume na waume bora duniani.

Nikapata rafiki, Joyce, mke wa rafiki wa mume wangu. Vitu vingi nilikuwa nikiendana naye lakini mwenzangu alikuwa akipenda sana kucheza muziki, na sehemu pekee aliyoipenda ni klabu, hakuwa muendaji sana lakini kwa mwezi lazima aende mara moja.

"Mara moja moja siyo mbaya,"
"Lakini ukienda klabu unacheza mwenyewe au?"
"Huwa najichanganya tu,"
"Kwahiyo watu wanakushika kiuno?"
"Kiuno tu! Mpaka kubambiwa,"
"Kha! Mimi siwezi, naona kama nitakuwa namsaliti mume wangu,"
"Kushikwa tu! Kufanya ndio kusaliti bwana,"
"Mmh! Siwezi kabisa."
Niliongea hivyo na Joyce ambapo katikati ya maongezi, alipigiwa simu, nikamsikia akiwa anongea...mwishowe aliniuliza,
"Anaweza kupitia hapa?"
"Nani?"
"Fundi wangu, wa kiume,"
"Mh! Sawa."
Basi alimwambia huyo fundi wake apitie nyumbani kwangu, kwavile alikuwa ni mgeni wa Joyce nilimruhusu. Baada ya kama dakika kumi na tano huyo fundi alifika. Alipofika huyo fundi ndio hapo kisa changu kilipoanza.

Alikuwa ni mwanaume fulani wa kawaida sana, hakumzidi mume wangu kwa chochote labda kitambi,




mume wangu alikuwa nacho cha wastani.
"Habari madam," alinisalimia hivyo
"Nzuri," kifupi nilimjibu
Basi waliongea na Joyce kisha alipotaka kuondoka aliniaga tena, sikumjibu chochote.
"Shosti mbona kavu hivyo? Au umemwelewa?" aliniuliza Joyce kishambenga
"Nimwelewe huyo kaka? Ah wapi,"
"Makasiriko ya nini sasa?"
"Basi tu, kwani ni nani?"
"Ni fundi, kabla hajaja nilikwambia, lakini kaka yuko vizuri, mrefu, mweusi, na unajua sifa ya wanaume warefu weusi?"
"Wana sifa gani?"
"Dudu..." alinijibu hivyo huku akionyesha mkono wake ishara ya kuashiria dudu kubwa.
Basi siku hiyo ilipita, kusema ukweli sikuweza kubishana na moyo wangu, yule kaka sijui ndio nilimpenda au nilimtamani, yaani nilijikuta nikimuwaza na kutafakari kilichonikuta hiyo siku. Nilipomuona yule fundi ni kama mwili uliishiwa nguvu, nilibaki nikiimtazama tu, ili nisimuonyeshe hilo nilijikuta nikimjibu kifupi tu.

Katika hali nisiyoitarajia, eti mume wangu alirudi siku hiyo akiwa na fundi yule aliyeniletea mchanganyiko wa mwili siku ile.
"Mke wangu, utachagua namna nzuri ya kupendezesha ukuta, huyu fundi atakusikiliza,"
"Sawa mume wangu." nilimjibu hivyo kisha nikambusu kwa hisia, alirudi kazini kuendelea na kazi.

Fundi huyo alijitambulisha jina lake kuwa akiitwa Basaula kisha akawa anataka kulijua langu, nikamdanganya kuwa naitwa Sheila, ni moja kati ya majina niliyokuwa nikiyatumia kabla hata sijaolewa pale nisipotaka mwanaume anifahamu.

Basi akaninyesha baadhi ya picha za 'Wolpepa' zilivyopendeza ukutani, nami nikachagua, sasa wakati nachagua mwenzangu sijui alikuwa akiwaza nini, si akadindisha, tena sijui hakuvaa boksa, nilimwangalia kwa macho ya wizi kisha nikaenda zangu chumbani,
"Njoo mchukue fundi wako huku kadindisha mshenzi huyu!" nikamtumia huo ujumbe Joyce, akacheka sana,
"Aliniambia kafa kaoza, na anataka akunyandue na atakwambia,"
"Nini? Athubutu aone!"
"Punguza munkari uko nyumbani kwako bwana,"
"Ngoja nikamtoe..."
Basi nilirejea sebuleni na siku hiyo nilivalia gauni langu lililokuwa pana tu, umbo lilinibeba, gauni hilo halikufika kwenye magoti. Palikuwa ni nyumbani kwangu kwahiyo sikuwa na presha,
"Kaka kuna wanawake wanajua kumpetipeti mume, kuna wanawake wanajua kubusu,



yaani wanambusu mwingine unasisimka mwingine,"
"Ndugu yako nikirudi salama jua Mungu ni mkubwa kaka."
Yote hayo aliyazungumza fundi Basaula akiongea na mtu kupitia simu, nilitamani kucheka, nilikumbuka pia yale maneno ya Joyce, nikapigia mstari Basaula alikuwa akinitamani.

Basi nilipokuwa jikoni niliandaa chakula huku nikiwa nimekubaliana na Fundi kuwa hizo Wolpepa za ukutani zitaletwa muda usio mrefu. Ghafla fundi akaniita,
"Umeniacha mwenyewe,"
"Niko jikoni naandaa chakula,"
"Nikusaidie lolote maana niko vizuri,"
"Hapana usijali,"
"Sasa siwezi kukaa bila kazi, nikusaidie hata kukata vitunguu,
"Sawa."
Nilimkubalia nikiamini kazi yangu itakwenda kwa haraka maana nilipanga kupika pilau la nyama ya ng'ombe. Fundi akaanza kukata vitunguu maji, akawa anajisifu kuwa yeye ni fundi wa vingi, akaanza kuongea mafumbo yake, kusema kweli moyo wangu ulikuwa una furaha tu kumuona, sijui hata alinivutia kitu gani. Nilishindwa kujizuia kumtazama usoni, jinsi alivyokuwa akiongea, vidole vyake, yaani ilikuwa ni upuuzi lakini kiherehere cha moyo sasa!
"Eh mwenyezi Mungu nionee huruma, nisaidie nisichepuke nampenda sana mume wangu." Nilisali hivyo moyoni
"Unajua kwenye maisha kuna mtu unakutana naye, unatokea kuvutiwa naye mpaka unajiuliza imekuwaje! Unagundua yuko na mtu hivyo kitu pekee unachoweza kukifanya ni kumfikisha tu..."
Aliongea hivyo ambapo nilijua kabisa nikimjibu nitakuwa nimeunga mkono huo upuuzi, nilikaa kimya huku nikiendelea na maandalizi.

Kuna kitu alikifanya jikoni hapo nikamfokea sana, alikuja kwa nyuma na kunikumbatia kisha akanibusu shingoni, kwakweli nilisisimka lakini nilijikaza na kumsukuma, nilimtukana mpaka mishipa ya shingo ilinitoka, nilimtolea maneno makali machafu mpaka nikajishtukia, sikuwahi kutukana hivyo,
"Samahani," nilimwambia hivyo
"Usijali, najua unanipenda, vyote vitanidanganya lakini sio macho yako,"
"Unaongea nini wewe!" nilipomjibu hivyo akanisogelea zaidi
"Macho yako tangu siku ya kwanza uliponiona, mimi pia nilikupenda sana, nikathubutu kumwambia rafiki yako akwambie lakini akasema umeolewa na hawezi kukuvunjia heshima,"
"Hebu toka!"
Nilijaribu kumkwepa kisha nikaondoka.
..



Nikaelekea chumbani ambapo niliwaza sana ni kwa namna gani nimtoe Basaula, nilishika simu yangu na kutaka kumjulisha mume, niliwaza sana nilipopata cha kumshauri nilimligia,
"Mke wangu kipenzi,"
"Eeh mume wangu, upo bize?"
"Kuna maandalizi nayafanya, tunaingia kwenye kikao,"
"Ooh sawa baba nilikumisi, uwahi kurudi,"
"Sawa mke wangu japo leo nitachelewa kidogo ila haitavuka saa mbili,"
"Sawa."
Nikawa mpole, nikampigia simu Joyce ili aje, akaniambia ana safari ya kwenda saluni na akitoka hapo atapokea mgeni hivyo itakuwa ni vigumu.

Basi nilitoka nje ambapo sikumkuta fundi, nilimtafuta nyumba nzima lakini nilimkosa, begi lake halikuwepo. Mara nikapokea ujumbe kutoka kwa fundi,
"Nimeondoka nitarudi baadaye, jamaa yangu aliyetakiwa kuja na mzigo amekwama." swali la kwanza nililojiuliza ni kwamba alitoa wapi namba yangu mpaka akanitumia huo ujumbe, kabla sijakaa sawa ndio Joyce akanipigia,
"Shosti kuniita haraka hivyo vipi?" aliniuliza Joyce
"Mwenzangu wee! Huyu fundi wako sijui ana majini, yaani akiwa tu karibu nakuwa sijielewi,"
"Wee! Nimempa namba yako, aliniambia aliondoka bila kuaga,"
"Ooh! Shosti mbona hatari, kusema kweli sijui hata nifanyeje,"
"Kwani vipi! Umempenda?"
"Hata sielewi, hivi hushangai kanibusu shingoni na nikajisikia vizuri kabisa, kwakweli siwezi kumruhusu aje tena,"
"Jamani, mapenzi mabaya,"
"Nitakuwa ndio nimempenda?"
"Ila jikaze kipenzi, ndoa muhimu, sio kwamba mimi hainitokei, hunitokea ila mume ni mume, ukichezea ndoa unaweza kuteseka sana,"
"Shosti umeongea, maana yule angenibananisha hata ndani humuhumu ningempa, bora hata alivyoondoka..."
Basi nilipiga soga na Joyce kisha nikakata simu utafikiri mimi ndio niliyepiga. Nikaingiza mkono kwenye kei yangu na kuutoa, tayari nilikuwa nimeshaanza kuchafuka.

Baada ya sekunde kadhaa, nikahisi nainuliwa, mwanzoni nilijua tetemeko la ardhi.
"Hello madam!" nilishtuka kusikia hivyo mpaka kelele ya uwoga niliitoa
"Usiogope bwana," nilipoisikia hiyo sauti ndio nikajua kuwa ni fundi Basaula. Akatoka chini ya sofa huku akiwa amedindisha kabisa tena waziwazi, nilimwangalia kwa kuibia huku nikiwa natafakari kuwa, kumbe yale yote niliyobwabwaja kwenye simu aliyasikia,
..

MWISHO





Blog