Search This Blog

Sunday, July 24, 2022

DILI LA X

  

MTUNZI : GEOFREY MALWA



Mh! Maisha majanga. Kwani waliofanikiwa walifanyaje? Nitaishindaje hii roho ya kutamani maisha mazuri na wakati sina uwezo nayo? Niuze mwili? Hapana, nifanye nini sasa? Maana wengi husema mwanamke pesa imewekwa katikati ya mapaja yake.

Nilijiheshimu sana ila tamaa ya maisha mazuri ya kifahari ilikaribia kuvunja ngome ya heshima niliyojijengea muda mrefu. Nilikuwa nikitamani sana nilipoona mwanamke ana gari, nyumba na anaendesha maisha yake akiwa hana shida yeyote. Niliona wivu mno na mpaka wakati mwingine nilikufuru Mungu kwa kumkosoa eti ni bora ningezaliwa kwenye maisha ya kitajiri.

Nilichovaa nilikichukia, nilichokula, aina ya marafiki na hata mpenzi niliyekuwa naye, vyote havikuupendezesha moyo wangu. Nilifahamu maisha ya kifahari yanaletwa na pesa lakini hiyo pesa ndiyo iliyoniumiza kichwa. Kwa sisi wanawake kama sio kwa kumpata mwanaume mwenye hela basi kuuza mwili, na kama sio hivyo vyote kwakweli jasho mpaka la mpododo litakutoka, hutokuwa na tofauti na wanaume katika utafutaji, ndio mimi sasa nilikuwa hivyo.

Mpenzi wangu alikuwa akiitwa Domi, alinipenda sana, alinisifia kila siku lakini sikuhitaji kusifiwa, nilichohitaji ni pesa. Alijitahidi kuonyesha ufundi kitandani lakini akili yangu ilikuwa ikiwaza ni kwa namna gani naweza kupata pesa nibadilishe maisha yangu. Alizama chumvini bara na pwani lakini ni kama alikuwa akinyonya miguu yangu tu, na sikuwahi kufika kileleni kila tulipokutana maana hisia zangu hazikutulia.

Katika pitapita zangu kwenye mitandao ya kijamii, ilikuwa ni Instagram, huwa ni mvivu sana kusoma jumbe ninazotumiwa, lakini siku hiyo nikawa nazipitia, ujumbe wa saba kuufungua ulikuwa wa Makastep, jina hata sikulielewa sana lakini aliandika hivi...
"Unaweza ukawa tajiri ndani ya siku moja lakini lazima upitie mambo magumu sana, kama uko tayari nijulishe..." akaandika na maasiliano yake. Akili ya tamaa ya pesa ikaanza kunitafuna taratibu, nikachikua namba zake, akaunti yake aliweka private kwahiyo sikuweza kuona yaliyomo.

Nikaanza kuwasiliana na Makastep, kwa jinsi alivyokuwa akiongea ni wazi lugha ya kiswahili kwake ilikuwa tabu kidogo. Akasema tukikutana itakuwa rahisi kunielezea kuliko kupitia simu.

Tukahamia Whatsapp. Tukafahamiana kwa picha, kumbe alikuwa ni mzungu. Nikashangaa, sikutegemea. Ilipopita miezi mitatu tukiwa tunawasiliana tu, tukapanga kuonana, sehemu nilichagua mimi japo aliniambia nisiogope kuhusu pesa hata nikitaka tukazungumzie Dubai.

Basi nikachagua hoteli fulani ya nyota tano na niliweka muda wa asubuhi ili iwe salama kwangu. Tukaonana vizuri, hakuisha kunisifia huku akisema kuwa hajakosea kichagua maana wengi wanavyoonekana Instagram hawapo hivyo kiuhalisia.
"Kwako maisha mazuri unayatafsiri vipi?"
"Kumiliki vitu vya thamani, nyumba, gari..." Nilipomtajia hivyo alicheka sana
"Nyumba na gari bado ni umasikini, akili yako itanuke ufikirie vitu vya thamani zaidi,"
"Kama vipi?"
"Hivyo ulivyovitaja ninaweza nikakupa hapahapa kabla maongezi yetu hayajaisha."
Basi alinielezea yeye kwa ufupi kuwa anatokea Ughaibuni ila hapa nchini ni kama wakala. Aliniambia mambo mengi bila kunieleza kiini cha sisi kukutana na vipi nitavuta mkwanja mrefu.

Basi akachukua simu yake kisha akaiplei video ya X, nikataka kukataa kuiangalia,
"Usijali, angalia mpaka mwisho."
Basi nikakomaa, ilikuwa ni video ya kiswahili kabisa, walikuwa wanaongea kiswahili, yaani nilishangaa maana nilijua waswahili huwa zinavuja zile za kujirekodi na sio kama hizo ambazo kuanzia kwenye kamera yake mpaka aina za picha zilizopigwa zilikuwa za hatari. Kwakweli ilikuwa ni video iliyosisimua sana.
"Unawajua hao?"
"Hapana,"
"Mmoka anamiliki hoteli kubwa sana hapa mjini, huyo mwanaume ndio kabisa ana hoteli Dubai. Hawana shida ya hela kwa kucheza hiyo video tu." Niliposikia hivyo nilinywea, nikacheze picha za ngono! Kweli? Nilibaki nikiwaza kabla ya kuongea chochote,
"Sio lazima na sio watu wote wanafaa, kama utakuwa tayari basi utanijulisha. Vipi! Nikupe gari la kutembelea? Unaweza kwenda nalo popote pale mpaka utakaponipa jibu hata kama jibu litachukua mwaka mzima,"
"Nitakujibu, ila gari hapana."
Akatoa kama milioni mbili na kutaka kunikabidhi zikiwa kwenye bahasha, nikakataa, bado akili yangu haikuwa sawa,
"Utacheza na mtu mmoja kwa kurudia naye mara tano ndani ya mwezi, baada ya hapo, hii hoteli tuliyokutana yenye hadhi ya nyota tano itakuwa ni yako, utapewa nyumba mbili za kifahari, gari tatu utakazochagua na pesa bilioni ishirini, vyote hivyo utavipata kabla ya kukamilisha kazi,"
"Mh! Yaani hao wawili wamechezea wapi?"
"Hapa hapa Tanzania na siwezi kukwambia mpaka uwe mmoja wao."
Basi siku hiyo niliziacha zile milioni tano na kuondoka zangu mpaka nyumbani. Niliwaza sana hilo jambo.

Ni kweli maisha mazuri niliyataka lakini kucheza x lilikuwa ni suala lingine kabisa. Basi nikaanza kuashirikisha baadhi ya watu kuhusu hilo jambo kwa kuwauliza maswali ya mtego, wengi walijibu kuwa wangeenda vizuri tu, lakini nilihisi hawakumaanisha.

Nilikuwa njia panda, katika maongezi yangu na Makastep, nikajikuta nahitaji kumzoea zaidi ili nijue ukweli wa alichokisema. Siku moja alinichukua na gari lake mpaka nyumbani kwake. Alikuwa na familia yake nzuri tu, nyumba kubwa ya kifahari, magari yalijipanga kama kumi hivi ya gharama,
"Hongera sana, una maisha mzuri,"
"Haya? Unaweza kuyapata mara mbili yake,"
"Hivi kwanini ulinichagua?"
"Kwasababu una muonekano mzuri,"
"Mh! Haya bwana."
Tuliongea hayo tukiwa nje ya nyumba yake sehemu ya wazi iliyokuwa na zuria la rangi ya kijani. Alikuwa na watoto wawili wa kike. Nilitamani sana hayo maisha.

Basi tulipokuwa kwenye gari akinirudisha nyumbani, aliniambia kuna mahali anapitia kisha ndio anipeleke, takaenda wote. Ilikuwa ni hotelini, kumbe alikuwa anakwenda kumpa cheki ya bilioni arobaini jamaa mmoja hivi ambaye alifurahi na kumshukuru mpaka kupiga magoti akilia kabisa.
"Yule ulimpa dili?" Nilimuuliza Makastep tukiwa tumesharudi garini.
"Ndiyo, amekamilisha kazi yake jana,"
"Sawa."
Basi akanirudisha mpaka nyumbani, yeye akashuka na kuita usafiri mwingine, gari akaniachia aina ya BMW ile tuliyokuja nayo.
"Hii nakuachia, ukiihitaji nenda nayo popote..."
"Sasa, sikutaka iwe hivyo..."
Dakika kumi na tano mbele gari ikaja kumchukua kisha akandoka. Gari lilikuwa zuri kweli, kuendesha nilijua hivyo nikalijaribu kidogo. Zile dakika nilizotumia kuketi kwenye kile kiti cha gari nilihisi kama nimetimiza moja ya matamanio yangu.

Makastep alindelea kuniweka karibu ambapo niliona akiwa anaalipa watu mabilioni ya pesa baada ya kukamilisha kazi, na sijawahi kusikia hao watu wakiongelewa vibaya au kujulikana kwa namna yeyote. Nikaanza kushaishika kutokana na pesa nyingi zinazotolewa.

Nilipokubali, Makastep alifurahi sana. Akanipeleka hospitari ambapo nilipimwa vipimo vyote, majibu yalivyotoka alizidi kufurahi mpaka nikamshangaa,
"Unajua katika hii kazi huwezi kuifanya kama umeathirika au kuwa na magonjwa yeyote ya ngono...

VIDEO YANGU YA X YA KWANZA.

MWISHO












Blog