Search This Blog

Sunday, July 24, 2022

SEX MACHINE

   

MTUNZI : GEOFREY MALWA



Richa ya dunia kuwa na mazuri ambayo hutufanya tuyafanye kuwa ni sababu za kuishi, yapo mabaya ambayo yanaweza kukufanya uone maisha hayana thamani. Nakukaribisha katika chombezo hili ambalo mkasa wake utakufunza mengi mno ila pia utaburudika kwa msisimko uliofichwa kwenye maandishi yake.

“Kaka una uhakika?”
“Ndiyo, usijali mdogo wangu, jamii haitokuelewa,”
“Lakini unalijua tatizo langu,”
“Haturuhusu alifahamu, unafunga naye ndoa kisha kila mmoja anakaa kivyake, tunamlipa pesa tu,”
“Kweli pesa inaweza ikamaliza kila kitu?”
“Ndiyo, tunamtafuta mwanamke mrembo, na hawezi kukataa mbele ya pesa,”
“Sawa.”
Mika na Niki walizungumza hivyo ambapo Mika ndiye aliyekuwa mkubwa, Niki alimsikiliza kaka yake kwa umakini na kukubaliana naye juu ya mpango alioshauriwa.

Jongoo kutopanda mtungi, dudu mkufu, hivyo vyote viliwakilisha tatizo alilokuwa nalo Niki. Dudu lake halikuwa na uwezo wa kusimama. Hali hiyo ilimtesa sana na kumfanya kuwa na hasira muda wote kwani alihisi amepungukiwa kitu kikubwa sana. Kuna wakati alitamani kujiua ila Mika alisimama kidete kumshauri na kumtafutia wataalam wa saikolojia mpaka afya yake ya akili ikarudi kawaida.

Niki alichobarikiwa ni uzuri, alikuwa ni mwanaume ambaye kama ukimwangalia vibaya ungeweza kudhani ni mwanamke aliyeota ndevu. Ila uhendsam wote huo aliuona ni sifuri kama hakuweza kulitetea jina la Niki kitandani.

Basi haraka zilianza, akatafutwa msichana mrembo mno, akaelekezwa mpango mzima bila kuwekwa wazi tatizo la Niki. Msichana huyo aliitwa Lidya, alikubali kwa kuigiza kuwa mke wa Niki. Lidya alikuwa ni msichana wa viwango vyote, idara zote nyeti za kike alijaaliwa. Sijui hipsi, makalio, urefu, sura nzuri, rangi mujarabu. Hakuwa mnene wala mwembamba.
“Kaka natamani kama nisingekuwa na tatizo, huyu mwanamke nimempenda kweli,” alisema Niki
“Hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho,”
“Nashukuru kaka.”
Taratibu zote zilifuatwa, ndoa ikafungwa, cheti kanisani wakapewa. Ikatambulika kwa jamii kwamba ni ndoa halali. Kibubu cha Lidya benki kilishajaa, hakuona ugumu wowote.

“Kwahiyo hujajua kwanini jamaa ameamua kufanya maigizo?” alihoji Danso
“Sijui kwakweli, ila tamu yangu simpi hata anishikie risasi,” alijibu Lidya
..


“Najua, ila nimetafakari sana,”
“Usijali rijali wangu, ili mradi pesa imeshaingia,”
“Kweli hilo ndio muhimu.”
Lidya na mpenzi wake walikuwa wakijadili sababu iliyojificha nyuma ya maigizo hayo bil akupata majibu sahihi. Niki alikuwa kwenye nyumba yake ambapo Lidya aliishi kwa muda wa mwezi mmoja. Kwa muda huo wa mwezi mzima, Lidya hakuwahi hata kuhisi tatizo la Niki.

Lidya jambo lake alilitimiza, kwahiyo baada ya mwezi walikubaliana kuwa siku yeyote akihitajika basi iwe rahisi kwake kufika maana ni mke halali kwenye makaratasi. Lidya kwake hakuona kikwazo chochote, kwahiyo suala ya kuendelea na uhuru na maisha yake lilikuwa mikononi mwake Lidya,
“Ila Niki, wewe ni mwanaume mzuri, kwanini umeamua kuigiza haya yote,” alihoji Lidya kwa upole wakiwa chumbani
“Sio kila kitu kwenye dunia kipo kama kinavyoonekana,”
“Unamaanisha nini?”
“Iko siku utaelewa tu,”
“Mh!”
“Nikuulize swali?”
“Niulize chochote?”
“Kwa jinsi ambavyo tuko wawili tu humu ndani, ungeweza kuniruhusu nikunyandue?”
“(Kicheko)”
“Mbona unacheka?”
“Sijui…” alijibu Lidya huku akiendelea kucheka, alikuwa ni mwanamke mzuri aliyejaa ushawishi kila idara. Kwa jinsi Lidya alivyojiweka, ni kama alikuwa akimtega Niki japo haikuwa ile mitego ya moja kwa moja. Basi muda wa kulala ulipofika Niki aliondoka na kumwacha Lidya chumbani, walikuwa wakilala vyumba tofauti.

Basi siku hiyo asubuhi na mapema Niki aliamshwa na hodi, alikuwa ni mlinzi wake,
“Mchungaji anahitaji kuonana na wewe,”
“Mchungaji?”
“Ndiyo,”
“Hebu mruhusu.”
Niki alishangaa huku akiwa na shauku ya kumuona huyo mchungaji.

Huku upande wa Lidya akiwa na Danso, waliketi sebuleni kwenye nyumba yao mpya waliyopanga kwa zile pesa za dili la kuolewa feki.
“Bebi ulisema kuna ubuyu unao,”
“Husahau tu!”
“Niambie, tena ulisema unamhusu Niki,”
“Aisee, kumbe yule jamaa jongoo hapandi mtungi,”
“Hasimamishi?”
“Ndiyo, kuna jamaa kaniambia hivyo, alisoma naye sekondari, si unajua jinsi dunia ilivyo ndogo,”
“Kweli?”
“Ndio hivyo, mpaka kuna msichana alithibitisha, alipigiwa simu, unaambiwa jamaa tangu azaliwe yuko hivyo,”
“Anhaa, ndio maana alitaka afeki ndoa ili jamii imuone yuko sawa,”
“Ndio hivyo.”

..


Tukirudi huku kwa Niki, siku hiyo alipokea taarifa ya kitofauti sana, hakuamini kwenye masikio yake, ni kama alikuwa akiota vile,
“Mchungaji unayoyaongea ni ya kweli?”
“Ndiyo kijana wangu, lakini kama nilivyokwambia, pindi uponyaji utakapoupata usihangaike na mbaya wako japo lazima utamjua hapo baadaye,”
“Yaani mchungaji unamaanisha kuna mama ambaye aliniroga kisa tu nilikuwa mtoto mwenye muonekano mzuri kuliko mwanaye?”
“Ndiyo, hiyo ilimfanya ajisikie vibaya sana, akaamua kukufunga,”
“Atakuwa ni nani huyu?”
“Jali kwanza kupona, ukiwa mtu wa kuendekeza visasi pengine hata Mungu anaweza aikuponye maana atakuponyaje mtu mwenye mawazo ya kuangamiza?”
Niki alikubali kuombewa ili hiyo hali imuishe, mchungaji alianza maombi kwa muda huo ambapo alimwambia Niki kuwa aamini lazima atapona na maombi yatakuwa ya siku tatu, alifunga mchungaji bila kunywa wala kula chochote. Siku tatu zilipopita Mungu alionyesha ukuu wake, Niki akapona kabisa, mtu wa kwanza kumshirikisha alikuwa ni kaka yake, tena asubuhi na mapema baada ya kuona hiyo hali, wa pili akawa ni mchungaji. Ilikuwa ni furaha isiyokuwa na kifani kwa Niki, yaani kama kipofu aliyepewa uwezo wa kuona baada ya kumda mrefu.

Akiwa kwenye hiyo furaha, alipigiwa simu na Lidya, haikuwa kawaida maana makubaliano yalikuwa mpaka Niki ampigie simu Lidya,
“Hello Lidya,”
“Mimi ni mkeo jamani hendsam,”
“Sawa mke wangu niambie,”
“Nakuja, nimekumisi, nikuone tu mume wangu,”
“Sawa karibu. Hapa ni kwako.”
Lidya hakumshirikisha Danso kama anataka kwenda kumjaribu Niki, katika maisha yake hakuwahi kukutana na mwanaume asiyeweza kusimamisha dudu. Alitaka akajioneee mwenyewe, hakujua kuwa Niki alishapona.

Siku hiyo Lidya na lile umbo kama mnyarwanda alilivalia skinitaiti nyepesi na blauzi. Yaani ile skinitaiti iliyoonyesha mpaka mistari ya nguo ya ndani.

Niki alivalia boksa nne zilizombana, alificha kabisa dudu lake ili aendelee kuonekana kama mwanzo. Alimwangalia kwa macho ya matamanio Lidya mpaka kuna muda alishindwa kufanya hivyo kwa siri,
“Wewe inaonekana unapenda sana makalio eh?” Lidya alihoji hivyo kwa uchokozi tu
“Hapana,”
“Mbona unaniangalia kama unayatamani,”
..
..



MWISHO






Blog