Search This Blog

Sunday, July 24, 2022

MKE WA PILI

 



MTUNZI : GEOFREY MALWA




Kwa majina naitwa Mima Lwahidi. Nina umri wa miaka ishirini na mbili. Sikuwa na haja ya kuambiwa kuwa mimi ni mzuri, nilijijua. Katika jiji la Dareslaam, walijipanga wanaume wengi wenye mvuto wa kila aina, wote walihitaji kuwa nami, lakini kwa upande wangu sikuona hata mmoja ninayeweza kumpa nafasi.


Mwaka wa pili ndio niliuanza katika chuo kikuu cha Daresalaam, niliuhesabu ni mwaka wenye baraka kwani sikuwa na somo la kurudia mtihani.


Rafiki yangu Mwanne, alikuwa ni bingwa wa kutazama video za pilau, na kila aliloliona alilijaribu kwa mpenzi wake. Sikuwa mfuasi wa kuangalia hizo video ila siku moja alinilazimishia kuangalia,

“Wewe! hilo dude lote linazama kwa mwanamke?” nilishangaa nilipoiona

“Ndio, cheki anavyokojoa sasa,” alinijibu Mwanne

“Mh! Haya sio maji?”

“Ndio kukojoa kwenyewe huko,”

“Mtu unatoka maji?”

“Ndio hivyo, wewe kibanie tu mwisho wa siku kioze,”

“Ebu toka huko, lakini wanaume weusi wana makitu jamani!”

“Tena waogope sana wanaume wembamba warefu, nyama zote zimekusanya huko chini,”

“Kweli eeh?”

“Habari ndio hiyo…”

Maongezi hayo yalinijuza jambo fulani, kusema ukweli nilikuwa mshamba wa mapenzi, sikuyaendekeza kwasababu sikuona raha yake zaidi ya kupeana mawazo ukizingatia wengine familia zetu zilitutegemea.


Nikiwa bwenini, alikuja Damiani, ndiye mwanaume pekee niliyekuwa nikipiga naye stori, alikuwa ni shemeji yangu kwa Mwanne. Naye alishawahi kunitongoza ila nilimtuliza na kumwelekeza vyema maana alipendwa sana na rafiki yangu. Sikuwahi kumwambia Mwanne ila nilihakikisha hamsaliti rafiki yangu.


Damiani tulipomkaribisha walikumbatiana na Mwanne wenyewe mapenzi motomoto, alipotulia sasa,

“Aisee kabla sijasahau, nina ujumbe wako hapa,” alisema Damiani

“Ujumbe gani?”

“Upokee kwanza,”

“Umetoka wapi, nikipokea bomu je?”

“Haujatoka kwa mwanaume, upokee,”

“Kwani mimi naogopa ukitoka kwa mwanaume?”

Basi niliupokea huo ujumbe ambapo ilikuwa ni karatasi nyeupe iliyobanwa kwa pini,

“Naomba tuwe marafiki, nimekuchunguza nyendo zako tangu ukiwa mwaka wa kwanza” Hiyo karatasi iliandikwa ujumbe huo halafu chini yake palikuwa na namba za simu za mitandao mitatu.

“Huu ujumbe kakupa nani?” niliuliza nikiwa makini kidogo usoni

“Mama fulani hivi, yule ambaye huwa anakuja na gari nzuri hivi,”

“Yule ambaye yuko mwaka wa mwisho?”

“Huyo huyo, mweupe hivi,”

“Watu huwa wanamsema kuwa kafuata nini chuoni wakati mambo yamemnyookea?”

“Ewaah! Huyo huyo, kwani anasemaje?”

“Hapana.”

Nilikatisha maongezi kwani sikutaka kuweka wazi kwanza, nilijiuliza maswali mengi mama mwenye pesa kama yule aombe urafiki na mimi! Bora hata ningekuwa na akili sana ningesema atataka nimsaidie kwenye mitihani, ufaulu wangu ulikuwa wa kawaida tu.


Basi nilitoka nje ya bweni na nikatafuta sehemu nzuri iliyotulia, ile karatasi niliishikilia mkononi, nikachukua simu yangu na kuandika namba ya mtandao niliokuwa ninautumia kisha nikampigia, alipopokea tu, baada ya kusema “Hello!” alinijua,

“Bila shaka ni Mima sio?” aliniuliza hivyo

“Ndiyo mama,”

“Usiniite mama, niite dada,”

“Nikuite dada nani?”

“Dada Love,”

“Sawa, ujumbe wako nimeupata ila siamini kama ni wewe ndio umenitumia,”

“Ni mimi, nasubiri jibu, umenikubalia ombi langu?”

“Ndiyo, jamani kwanini nikatae?”

“Nashukuru sana, uko wapi muda huu?”

“Niko chuoni,”

“Natamani kukuona nina mengi sana ya kuongea na wewe…”

“Mimi pia, kesho utakuja chuo,”

“Naachaje na wakati sababu za kuhudhuria chuo zimeongezeka,”

“Kweli?”

“Ndio, ukiachana na masomo sababu yangu nyingine ni wewe…”

“Ahsante, ila nina maswali mengi ya kukuuliza,”

“Usijali, kesho itafika.”

Basi nilikata simu yangu kisha nikaiweka kifuani, sijui hata nilikuwa nikifurahia nini.


Kumbukumbu ndogo ndogo zikaanza kunijia Kichwani kuhusu dada Love. Alikuwa ni mwenye kuniangalia sana tangu nimeanza kumuona. Kuna siku alishawahi kutununulia chakula cha mchana na tulipomshukuru wala hakuonyesha kutuchangamkia.


Basi nilikuwa na maswali mengi sana hata usiku sikulala vizuri utadhani niliambia hiyo kesho nitakwenda mjini. Nilikuwa na shauku kubwa ya kuongea na dada Love.


Kweli asubuhi ilifika na nilivalia vizuri siku hiyo, kichwani nilijifunga kilemba kwani nilijua nywele zangu zingeniabisha, marashi niligundua yameisha baada ya kutikisa kopo lake, nilikwenda chumba cha jirani ambapo niliwakuta bado wamelala, niliwaamsha kisha nikawaomba wakanipa, nilipojipulizia nilienda kuonana na dada Love ambaye alikuwa ameshawasili chuoni na alikuwa kwenye mgahawa wa chuo…




Dada Love aliponiona tu, alinyanyuka huku sura yake ikiwa kama mtu aliyemuona ndugu yake waliyepotezana miaka mingi, nilipomkaribia alinikumbatia na kunibusu kwa furaha mno,

“Unalala sana na wewe, mzima?” alisema hivyo

“Niko salama hofu kwako,”

“Mimi ni buheri wa afya kama unavyoniona…”

Basi niliagiza nilichotaka, niliambiwa nisiwaze kuhusu kulipa, nile ninachotaka.


Tulipomaliza, dada Love alitoa wazo ambalo nami sikulipinga, alisema kwavile ni siku ya kwanza katika mahusiano yetu basi twende sehemu tukayafutahie maisha, nichague popote,

“Twende sehemu yeyote nzuri,”

“Itaje jina,”

“Kusema kweli mimi sio mtembezi kwahiyo hata maeneo mazuri siyajui, labda tutafute,”

“Ooh! Hilo nalijua, lakini nina wazo,”

“Lipi hilo?”

“Twende nyumbani kwangu, kuna sehemu nzuri tulivu tunaweza kuongea mambo yetu mengi…”

“Sawa.” Nilikubali kisha tukaongozana mpaka kwenye gari, tulipokuwa tukitembea pamoja mimi nilitangulia mbele kidogo,

“Mh! Mrembo huyo!” alisema hivyo baada ya kuona makalio yangu yanavyotikisika, japo niliyabana na suruali lakini ulaini wake ulijidhihirisha

“Dada Love sitaki, tangulia wewe!”

“Haya…” alipojibu hivyo alitangulia yeye,

“Mh! Mh! Mh..!” nilimlipizia kwani na yeye japo alivalia ushungi ila makalio yalijitokeza kwa mbali. Tukajikuta wote tukicheka huku tukiingia ndani ya gari. Watu walitushangaa maana hawakujua urafiki wetu umeanza lini mpaka kumfikia kuchangamkiana hivyo.


Sikuamini hiyo mitaa ya mbezi ufukweni tulivyoianza, hizo nyumba za kifahari, ama kweli mahali walipo matajiri wala hauna haja ya kuumiza kichwa kupajua. Mwishowe tuliingia kwenye mjengo fulani wa maana baada ya kufunguliwa geti na mlinzi,

“Unaishi hapa?”

“Ndio nyumbani kwetu, mimi na wewe,”

“Mh! Kivipi?”

“Nyumbani kwangu ni kwako, karibu sana.” Alifungua mlango wa gari kisha akazunguka upande wangu na kunifungulia mlango.


Humo ndani sasa, ndio zile nyumba ambazo huwa naishia kuziona kwenye filamu tu. ndani ya nyumba hiyo hakukuwa na mtu mwingine yeyote zaidi yake na mlinzi getini. Niliziona picha zake na mume wake aliyekuwa amekwenda umri kidogo.


Alinipeleka sehemu ambayo waliitengeneza kama vile ufukweni, palikuwa na vile viti vitanda vya kulala, mbele yake bwawa la kuogelea. Basi pembeni tukiwa na ‘waini’ maongezi yaliendelea,

“Kwanini mimi?” nilimuuliza

“Kwasababu wewe ni msichana mrembo, unajitambua na kikubwa zaidi nimekupenda naomba niseme tu ukweli,”

“Ahsante, nakupenda pia jamani,”

“Nafurahi kusikia hivyo,”

“Ni kweli ulikuwa ukinifuatilia tangu mwaka wa kwanza?”

“Ndio,”

“Kwanini?”

“Nilikuwa nakuchunguza kama unafaa,”

“Kuwa rafiki yako?”

“Ndiyo, mimi na mume wangu,”

“Mume wako yuko wapi?”

“Yuko kazini, atarudi baadaye jioni,”

“Anhaa, hongera una nyumba nzuri, kusema kweli sijawahi kuingia kwenye nyumba kama hii,”

“Hapa sasa ni kwako, hata ukitaka kuhamia muda huu ni wewe tu, hapa kuna kila kitu, ulinzi, chakula, malazi na kila unachokitaka,”

“Kweli?”

“Ndiyo,”

“Hivi wewe dada malaika au?” nilijikuta nikiongea hivyo na kumfanya acheke.


Siku hiyo ilimalizika tukijuana tu, dada Love alikuwa ni mcheshi sana, nilitokea kumpenda. Tulipitia saluni kurekebisha nywele zangu na kucha. Alinifanyia manunuzi binafsi ya nguo na baadhi ya vitu nilivyomwambia maana aliniambia kuhusu hela nisiwaze kabisa.


Baadaye sana, yalikuwa ni majira ya saa moja jioni, alinirudisha na gari mpaka hosteli, nilimshukuru na nilipotaka kushuka alinizuia,

“Unaniagaje hivyo?”

“Jamani dada Love, haya njoo…” nilimkumbatia kama sekunde thelathini hivi,

“Nakupenda sana wewe msichana,”

“Nakupenda pia…”

Baada ya hapo akanibusu mdomoni kabisa, nikabaki nimeduwaa, kabla sijahamaki vizuri ulimi ukawa unapiga deki kwenye lipsi zangu zilizozubaa na kutengeza uwazi fulani, tulifanya hicho kitendo kama dakika nzima,

“Samahani, usinichukulie vibaya, nimekupenda sana na sijawahi kupenda mwanamke mwenzangu kwa kiwango hiki,” aliniambia hivyo

“Usijali…” nilimtuliza hivyo maana alishanganyikiwa kweli huku akiniomba msamaha,

Wakati akiwa ananiomba msamaha mimi nilimshika mkono kisha nikambusu mdomoni,

“Uwe na usiku mwema.” Nilimwambi ahivyo kisha nikashuka kutoka kwenye gari….





Mazoea kati yangu na dada Love yalizidi kiasi kwamba sikuweza kumficha lolote lililokuwa likiendelea iwe ni kuhusu mwili wangu au matatizo ya kifamilia. Alinisaidia kwenye mambo mengi sana, hata pindi sponsa wangu alipoghairi kunilipia ada mara baada ya kumkatalia kuanzisha mahusiano naye, dada Love alichukua hilo jukumu, tulipendana sana.


Nyumbani kwake palikuwa ni kwangu, ugomvi mkubwa niliokuwa nao juu yake, alihitaji sana nikaishi kwake nami nikawa nasita kufanya maamuzi.


Baada ya kupita miezi minne, yaani mazoea niliyokuwa nayo na dada Love yalipitiliza, suala la kumbusu mdomoni, sijui kucheza michezo ya njiwa na yeye, ilikuwa kawaida mno, ilikuwa nisipomuona siku moja najihisi vibaya sana, yeye ndio kabisa, tulitumia muda mwingi kuongea utadhani ni wapenzi, yaani mwanaume na mwanamke. Kuna muda mume wake alikuwa akimuonea wivu, lakini alipojua ni mwanamke naye alijikuta akiongea na mimi kupitia simu.


Mume wa dada Love aliitwa Chikawe, alikuwa ni mpole, mtaratibu, mwenye kufanya mambo yake kwa umakini mno, sikumzoea kwasababu nilishawahi kumuona mara mbili tu katika kipindi hicho cha miezi minne. Kila mahali atakapokuwa dada Love kuanzia saa moja kamili asubuhi mpaka saa moja jioni nami nilikuwepo.


Dada Love alinisaidia kuninyooshea ‘malekcha’ wote waliokuwa wakinitongoza na muda mwingine kuahidi kunifelisha. Kusema kweli nilipendeza mno, hizo nguo nilizokuwa nikivaa! Hizo nywele nilizokuwa nikibadilisha kila wiki! Dada Love alinipa kaburi mno, wanaume wengi walinimezea mate lakini sikuwahi kuwawazia hata sekunde.


***


Basi siku moja dada Love hakuwa mchangamfu kama nilivyomzoea, nilihuzunika moyoni kwani kusema kweli katika kipindi kifupi nilitokea kumpenda sana. siku hiyo alinichukua chuoni na kunipeleka pale samaki samaki. Sikuacha kumuuliza kuhusu mabadiliko hayo ya ghafla maana sikupenda kumuona akiwa katika hali kama hiyo.

“Mima,” aliniita hivyo, hakuwahi kuniita hivyo muda kidogo

“Abee kivuruge wangu,”

“Kuna jambo nataka unisaidie, ni gumu sana,”

“Lipi hilo, hakuna kitu ambacho siwezi kufanya kwa ajili yako, nakupenda sana,”

“Najua kuwa unanipenda ila hilo jambo linahitaji moyo wa ziada, naomba usihisi kama nakuvunjia heshima,”

“Hapana mpenzi wangu, huwezi kunivunjia heshima, niambie lolote, nakuhakikishia ukiniambia tu nitaanza kulifanya muda huo huo,”

“Unasema kwavile hujalijua bado,”

“Nijaribu, niambie halafu uone, mpenzi usilie…”

“Ni ngumu,”

“Hakuna jambo gumu mbele yetu kipenzi changu, tunapambana wote na kama kushindwa tunashindwa wote,”

“Sawa, jambo lenyewe ni hili…” nilikaa mkao wa umakini kumsikiliza, alishindwa kuniambia.


Baada ya kutumia kama masaa matatu hivi ndio dada Love alifunguka,

“Nahitaji uifanye kazi yangu kwa mume wangu,”

“Kazi yako? Kivipi?”

“Uwe MKE WA PILI,”

“Dada Love unamaanisha?”

“Ndio, ni jambo gumu najua lakini naomba unifichie aibu tafadhari,”

“Kwanini unataka niwe mke wa pili?”

“Kwasababu mimi nina tatizo, na sitaki mume wangu ahangaike kwa wasichana ambao watakuja kumuumiza baadaye, usifikiri simpendi mume wangu, nampenda sana ndio maana namtakia mema,”

“Dada Love una tatizo gani?” nilimuuliza hivyo machozi yakinitoka

“Tatizo kubwa tu, siku moja nitakuelezea yote,”

“Hilo tatizo linahusiana vipi na kuhitaji msaada,”

“Hilo tatizo ndilo linalonifanya nisiweze kufanya majukumu yangu, nakuomba Mima usikatae, nakupenda sana,”

“Dada Love, usijali, Hakuna jambo lisilopata suluhu, nakuahidi tutavuka salama,”

“Ahsante, ukikataa nitakuwa nimejiabisha sana,”

“Hapana, futa machozi, nashukuru sana kwa kutoa yako ya moyoni, nakupenda kipenzi changu.”


Basi nilimbembeleza dada Love siku hiyo ambapo niliporejea hosteli, nilibaki nikiwa na mawazo sana, yaani kuwakatalia kote wanaume ndio niishie kwenye penzi la mtu mzima tena mume wa mtu? Sikutaka kuamini, lakini kwa upande mwingine niliuona moyo wa kishujaa wa dada Love kuongea ukweli wake. Nilianza kuuvuta picha jinsi nitakavyokuwa na huyo baba, kwanza nilikuwa namuogopa japo ni mpole. Usiku huo ulikuwa mrefu sana.

“Najua huwezi kulala mapema, samahani mpenzi,” alinitumia ujumbe mfupi kupitia WhatsApp, yalikuwa ni majira ya saa saba usiku

“Nawaza sana,” nilimjibu

“Pole, ukinikubalia nitakuwa mwanamke mwenye furaha sana, nitajua mume wangu yuko katika mikono salama,”

“Usijali,”

“Vipi, umekubali nianze kufanya sherehe?”

“Sawa, lakini kwanza tukapime tujue afya zetu…”

“Hilo limepita.”

Dada Love alifurahi sana, alinipigia simu na tukaongea mno, kusema ukweli nilikubali ili kumridhisha dada Love,sikuju ahata huko mbele itatokea nini.


Kumbe mumewe hakuwa na taarifa za kutafutwa mimi, tulikwenda kjua afya zetu ambapo tuliongozana kwa pamoja pasi na mumewe kushtukia lolote. Wao walipima peke yao nami nikapima mwenyewe.

“Wote tuko salama,”

“Sasa, kama hajui mimi nitaanzaje?’

“Usijali, najua mume wangu anapenda nini, hamia nyumbani kwangu,”

“Halafu?”

“Utaanza kuvaa nguo za mitego, nitamfanya awe anashinda nyumbani ili akuone, najua anapenda nguo za aina gani na akiona nini lazima aingie kwenye kumi na nane,”



“Sawa.” Nilikubali hivyo ambapo nilimshirikisha Mwanne kwa maswali fulani ambayo aliyajibu kirahisi mno

“Hivi wale wasichana wanaotembea na watu wakubwa waliowazidi umri, huwa wanafikiria nini?” nilimchokoza hivyo Mwanne

“Hela, wala Hakuna kingine,”

“Lakini mapenzi wanasema hayachagui,”

“Ni kweli lakini wengi wao wanapenda sana hela,”

“Kwahiyo wewe unaweza kusuuzwa na baba mtu mzima?”

“Inawezekana, lakini mpaka vijana wote wafe,” nilicheka aliponijibu hivyo

“Kwanini?”

“Mara nyingi vijana ndio wanapiga kazi ya maana kitandani, sasa hao watu wazima shoo zao ni zile za kutotoa jasho,”

“Mh! Haya bwana,”

“Lakini kitu ambacho sio cha kawaida kwenye jamii yetu ni kwamba, kijana kutoka na mwanamke mkubwa maarufu kama ‘mashuga mami’ ila kwa wanawake sio jambo la kushangaza kutembea hata watu wenye hadhi ya baba zao…”

“Ila kweli, kwa mfano yule msanii alivyoolewa na marehemu Mene Renegadi.”

Kwavile sikuwa na watu wengi wa kuzungumza nao mambo yangu zaidi ya Mwanne, ilitosha jinsi Mwanne alivyokuwa akinijibu.


Wiki iliyofuatia nilihamia nyumbani kwa dada Love nikiwa na vitu vyangu vya kitaaluma tu. Zile nguo zote aliniambia niziache, nilifanya hivyo kwani nilijua suala la nguo ni la dakika chache tu akiliamulia.


Siku hiyo niliyofika, ndio siku ambayo dada Love alianza kutengeneza muunganiko kati yangu na mumewe. Nilimuogopa huyo baba kwani sikuwahi kuwaza kama ingetokea siku moja nikakubali kirahisi hivyo kutemewa mate mazito na baba kama huyo, alikuwa mkubwa sana kwangu.


“Kwavile huna nguo, shika hili gauni ulivae,” aliniambia dada Love

“Fupi hivi?”

“Wewe unaona mimi nimevaaje?”

“Mh! Sawa,”

“Utazoea tu, nyumbani kwangu inabidi usiwe mtu wa kuvaa nguo nyingi, usijibane,”

“Sawa, nimekusikia mpenzi wangu,”

“Mume wetu anakaribia kurudi, nataka ukaoge, ukishaoga, vaa nguo ya ndani ambayo unajua itaonyesha mistari kwa nje, nywele zako zibane kwa nyuma, usoni usijirembe sana,”

“Sawa,”

“Na wewe ndiye utakayeenda kumpokea leo.”

Dada Love alinipa maagizo hayo ambayo niliingia chumbani na kuanza kuyafanyia kazi.


Aliporudi mume wetu basi nilitoka nje kwenda kumpokea na gauni langu lililonikaa mwilini mtoto wa kike, sio siri kama ni umbo tu nilibarikiwa, yaani uzuri kwa kifupi, hilo sikupinga hata kidogo, hata mwanaume awe mgumu vipi kwangu lazima shingo izunguke.

“Nani tena?”

“Mima,”

“Ooh, sawa, karibu sana,”

“Ahsante dadi, pole na kazi na karibu nyumbani,” nilipomwambia hivyo nilimkumbatia kwa hisia sijui hata ujasiri niutoa wapi

“Ahsante…” baada ya kujibu hivyo nilitangulia mbele makusudi, nilijua kabisa ile nguo ya ndani haikuzuia chochote, makalio yalitikisika na nilimuonea huruma baba wa watu niliyeanza kumuita dadi.


Yalikuwa ni majira ya saa kumi na mbili na nusu. Alipokaribia sebuleni nililipeleka begi lake chumbani kwa dada Love ambako nilimkuta akiwa amejilaza kitandani. Ila dada Love alikuwa sio haba jamani, jinsi alivyojilaza tu na lile gauni lake fupi kama langu kasoro rangi,

“Nakuona mama mwenye nyumba,” alinitania hivyo dada Love

“Nipo nimejaa tele,”

“Umemuacha wapi mume wetu?”

“Yuko sebuleni…”

“Nenda kamchunguze kwenye zipu ya suruali yake, ukiona amedindisha basi ujue dawa imeanza kumuingia,”

“Sawa.”

Nilitoka na kurudi sebuleni ambapo macho yangu yalikuwa makini na pale kwenye zipu yake ya suruali, aisee utadhani dada Love alikuwa mtabiri, aliponiona tu alikunja nne kuficha hiyo hali lakini mimi nilikuwa nimeshaona mtuno wa rungu lake mpaka mzunguko wa kile kichwa chake, ni kweli alikuwa amedindisha.

“Dada anakuita,”

“Sawa.”

Dadi aliponyanyuka tu ndio nikashuhudia mtuno halisi wa rungu lake lililoonekana kuchachamaa misuli hasa.


Alipoondoka tu, kusema kweli nami hisia zilikuja kwa mbali, sikuwahi kuona kitu kama hicho katika maisha yangu, wakati nikiwa nawaza hivyo, mara dada Love alikuja hapo sebuleni, alinikalia huku akifurahi, aliponigeukia kama kawaida yetu, tukacheza mchezo wa njiwa, tulizigombanisha ndimi zetu kama kwa dakika nzima,

“Tutafumwa hapa,” nilimwambia dada Love

“Unaogopa nini bwana mimi naupenda sana huu mdomo wako,”

“Acha, ebu kaa hapa kwanza,”

“Enhee…za kumdindisha mume wako?”

“Mh! Hivi dada Love huyo mume mwenyewe ndiyo ana rungu vile!”


MWISHO




Blog