Search This Blog

Sunday, July 24, 2022

NIPE KONEKSHENI

  

MTUNZI : GEOFREY MALWA


Siku moja mmiliki wa Akaunti katika mtandao wa Kijamii wa 'Instagram' aliposti picha iliowaonyesha wanawake wengi walio na matatizo wakiwa wamepanga folani kubwa nje ya nyumba ya mganga, kila mmoja alikuwa na tatizo lake ila asilimia tisini na nane walikuwa wakisumbuliwa na wanaume zao. Pia kwenye hiyo picha yakaandikwa mawazo ya wanawake hao, watu walicheka sana katika kipengele cha maoni huku wanaume wakichagiza kwa utani kuwa ni wao tu ndio watakwenda mbinguni siku ya mwisho.
Ucheshi huo aliuamini Jini, mwanamke ambaye alikwenda kwa mganga kutatua shida zake. Huko alikutana na wanawake mbalimbali ambapo wengi walikuwa na matatizo ya kusumbuliwa na mapenzi. Walijipanga foleni wakiwa katika viti maalumu sehemu ya kusubiri, utaratibu ulikuwa ni kuingia mmoja mmoja kwa mtaalam, ukishamaliza anaingia mwingine.
Zamu ya Jini ilipofika, aliingia kwa mtaalam. Jini alikuwa na umri wa miaka ishirini na saba. Hakuwa na tatizo kwenye mapenzi yake, alijaaliwa mwanaume ambaye alimpenda na aliridhika naye.
"Naomba kiganja cha mkono wako," alsema mganga, Jini akaunyoosha mkono wake. Baada ya sekunde thelathini, mganga au mtaalam wa tiba asilia aliyejulikana kwa jina la Zungumawe, alitabasamu kisha akasema,
"Sijawahi kukutana na kesi ya hivi tangu nizaliwe, labda nikisikilize,"
"Mtaalam, nahitaji dawa ambayo mwanamke yeyote nikizungumza naye akubali ninachomwambia,"
"Kwanini mwanamke?"
"Kwasababu sihitaji kufanya uhalifu,"
"Nafahamu dawa nitakayokupa wengi sana huitumia kwa utapeli, kwasasa siitoi tena maana hata mimi nilishatapeliwa japo vitu vyangu vyote nilivipata,"
"Siwezi kutapeli, nakuahidi..."
"Kwanza niambie, wanawake utakwenda kuwfanyia nini na dawa nitakayokupa?"
"Sawa...iko hivi mtaalam..."

BAADA YA WIKI MBILI.

"Kwani hapa nimefikaje babu?"
"Usijali, uko sehemu salama,"
"Mbona hujavaa nguo..."
Alivamiwa Meri, msichana aliyekuwa akisoma kidato kidato cha sita shule binafsi, kwa kifupi alikuwa ni mtoto wa kishua.
Babu aliyeitwa Jenzuu ndiye aliyemvamia na kuanza kumnyonya lipsi zake. Meri alikuwa kama amepigwa bumbuwazi. Kila alichoambiwa alikubali, Meri alikuwa ni msichana mzuri sana, kuanzia kichwani mpaka unyayoni.
Umbo la kuombea mkopo
..
MWISHO





Blog